IQNA

Mashia wa Tanzania Waanza  kuadhimisha kuuawa shahidi Imam Hussein (AS)

18:55 - July 09, 2024
Habari ID: 3479096
IQNA - Katika hali ya kuanza kwa mwezi wa Hijri wa Muharram, Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Tanzania wameanza kuandaa ibada za maombolezo ya kuadhimisha kuuawa shahidi Imam Hussein (AS).

Misikiti ya Shia na Husseiniyah (ukumbi wa  kidini) katika maeneo tofauti huko Tanzania huandaa maombolezo ya Muharram ya kuadhimisha mwaka wa kuuawa shahidi Imam Hussein (AS).

Kwa mujibu wa Kituo cha Utamaduni cha Iran nchini Tanzania, Mashia wenyeji na wanachama wa jumuiya ya Khoja Shia Ithna Asharia wakishiriki katika maombolezo hayo ya kukumbuka kuuawa shahidi Imamu Husein (AS).

Mipango hiyo  ni pamoja na ukariri na hotuba katika lugha tatu, yaani Kiingereza, Kiswahili na Kiurdu.

Kundi la Khoja Shia Ithna Asharia Jumapili lilipandisha bendera ya maombolezo ya Muharram na kuzindua mfano wa Vita vya Karbala jijini Dar es Salaam.

 

Tanzania Shias Begin Holding Muharram Mourning Ceremonies

Tanzania Shias Begin Holding Muharram Mourning Ceremonies

3489046

 

 

captcha